Mahiga amesema kuwa Watanzania hao wamefukuzwa Msumbiji baada ya kubainika kuwa wanaishi nchini humo bila kuwa na pasipoti za kusafiria, vibali vya kuishi na kutofuata vigezo walivyokuwa wamepewa na mamlaka husika ya nchi hiyo.
Hayo ameyasema wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ugeni unaotarajiwa kuwepo nchini Tanzania wa Rais wa Uganda, Yoweri Museveni anayetarajiwa kufanya ziara ya siku mbili ya Kitaifa nchini Februari 25 na 26, 2017.
Rais wa Visiwa va Shelisheli, Mhe. Dannu Faure naye atawasili Tanzania kwa ziara ya siku mbili kuanzia Tarehe 27-28, februari mwaka huu
USIKOSE PIA HABARI HIZI.........
No comments:
Post a Comment