asali

mbogo

sawe tv

advertise

SLIDE MANENO


Usipitwe na chochote, tupo ili kukuhabarisha tembelea blog hii kila siku, pia usisahau ku subscribe youtube channel yetu ya sawe tv

Monday, March 13, 2017

Singano ameligawa kiroho safi goli alilofunga dhidi ya Mbabane Swallows

WINGA wa Azam Ramadhani Singano “Messi” amesema goli alilofunga dhidi ya Mbabane Swallows ni zawadi kwa mama yake aliyetangulia mbele za haki.
Azam FC, wameanza vyema kampeni yao katika Kombe la Shirikisho Afrika baada ya kushinda bao moja katika uwanja wao wa nyumbani Azam Complex jijini Dar es Salaam.
Baada ya mechi kumalizika, Singano aliiambia shaffihdauda.co.tz kwamba anafurahi sana pale anapocheza na kufanikiwa kufunga, kwa sababu inamuongezea kujiamini.
“Kila mchezaji ana jukumu la kufunga na kuisaidia timu pale inapozidiwa bila kujali anacheza nafasi gani uwanjani kama mimi,” amesema Singano.
Ramadhani Singano alianza kutamba na mabingwa wa zamani wa Tanzania Simba SC kabla ya kujiunga na Azam baada ya kutokea sintofaham ya kimkataba kati ya Singano na Simba.


No comments:

Post a Comment

MAKTABA YA MAGAZETI / NEWSPAPER LIBRARY....... SOMA HAPA MAGAZETI YA SASA NA YALIYOPITA

  • MAGAZETI.
  • Tree in field with blue sky.
  • MAGAZETIt