asali

mbogo

sawe tv

advertise

SLIDE MANENO


Usipitwe na chochote, tupo ili kukuhabarisha tembelea blog hii kila siku, pia usisahau ku subscribe youtube channel yetu ya sawe tv

Saturday, April 29, 2017

Baada ya kuwanyoosha Zenji, Himid ana haya ya kuwaambia Simba

Azam FC wamekuwa klabu gumzo sana katika siku za usoni, aina ya wachezaji walionao pamoja na uwekezaji ndani ya klabu hiyo, kuelekea pambao la Simba na Azam mtandao huu ulifanya mahojiano na kiungo wao mkabaji Himid Mao.
Kwanza nilitaka kujua kuhusu Mao anauchukuliaje mchezo kati yao dhidi ya Simba ambapo alisema “Simba ni timu kubwa kama ilivyo kwetu sisi na mechi itakuwa ngumu sana kutokana na ukubwa wa timu hizi mbili, haitakuwa mechi rahisi”.
Kwa siku za karibuni Azam wamekuwa wakiisumbua sana Simba ambapo mchezo wao wa mwisho Azam waliifunga Simba katika ligi kuu ya Tanzania na Himid bado anaona Simba itakumbana na upinzani kutoka kwa Azam.
Mao aliulizwa kuhusu ubora wa kikosi cha Simba ambacho wachezaji wa nje kama Laudit Mavugo, James Kotei wamejenga kikosi imara wakishirikiana na wazawa kama Kichuya, Ajib, Mkude na wengineo.
Mao aliambiwa achague wachezaji watatu kutoka kwa wapinzani ambapo alijibu, “Mimi siangaliagi mpira na sijui kuhusu wachezaji wa timu nyingine japo nina marafiki Simba, huwa naangalia kikosi chetu na naamini tutaibuka kidedea dhidi ya Simba”
Mao amesema japokuwa kocha aliyepo Simba kwa sasa Mcameroon Joseph Omog anaijua sana Azam lakini hiyo haitawazuia kuwafunga wekundu hao wa Msimbazi kama walivyofanya mara ya mwisho walipokutana.
Himid ambae anaukumbuka sana msimu wa mwaka 2012 mechi waliyoifunga Simba bao tatu uwanja wa taifa amesema kikosi chao kipo tayari kuwakabili Simba.
Mwisho Shaffihdauda.co.tz ilitaka kujua kuhusu inakuwaje yeye yuko bize na msichana wake wakati timu iko katika maandalizi ya pambano gumu dhidi ya klabu ya Simba ambapo Himid alijibu kama ifuatavyo.
Kwanza yule sio msichana wangu, ni mke wangu wa ndoa na ieleweke hivyo na kuhusu kukaa naye naweza kaa naye muda wowote, picha zinahifaziwa kwenye simu na kupost picha haimaanishi umepiga hapo hapo” alimalizia Himid


No comments:

Post a Comment

MAKTABA YA MAGAZETI / NEWSPAPER LIBRARY....... SOMA HAPA MAGAZETI YA SASA NA YALIYOPITA

  • MAGAZETI.
  • Tree in field with blue sky.
  • MAGAZETIt