asali

mbogo

sawe tv

advertise

SLIDE MANENO


Usipitwe na chochote, tupo ili kukuhabarisha tembelea blog hii kila siku, pia usisahau ku subscribe youtube channel yetu ya sawe tv

Wednesday, April 12, 2017

Baloteli Afanya Kituko cha Mwaka Uwanja wa Ndege....awaacha watu mdomo wazi...!!!!


KAMA unafikiria kuwa kuna siku Mario Balotelli ataacha vibweka, basi futa hilo akilini mwako. Hivi karibuni aliwaacha hoi maofisa usalama wa Uwanja wa Ndege nchini Ufaransa, baada ya kuingia mlangoni kwa ‘style’ ya kuserereka kwa magoti.

Tukio hilo lilitokea baada ya kuiongoza timu yake ya Nice kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Lille.

Nice walikuwa wameshapachikwa bao moja na Lille, lakini mtukutu huyo alisawazisha kabla ya kuongeza jingine.

Wakati kikosi hicho kikiwa uwanja wa ndege baada ya safari hiyo ya kuwafuata Lille, Balotteli alitumia magoti yake kuserereka na kupita katika mlango waliokuwa wamesimama walinzi.

Kituko hicho hakikuwavunja mbavu wachezaji wenzake pekee, bali hata walinzi hao ambao walithibitisha ‘wendawazimu’ wa Muitalia huyo.


No comments:

Post a Comment

MAKTABA YA MAGAZETI / NEWSPAPER LIBRARY....... SOMA HAPA MAGAZETI YA SASA NA YALIYOPITA

  • MAGAZETI.
  • Tree in field with blue sky.
  • MAGAZETIt