asali

mbogo

sawe tv

advertise

SLIDE MANENO


Usipitwe na chochote, tupo ili kukuhabarisha tembelea blog hii kila siku, pia usisahau ku subscribe youtube channel yetu ya sawe tv

Saturday, May 6, 2017

BAADA YA PURUKUSHANI YA MUDA MREFU HATIMAYE TFF WATOA MAAMUZI RASMI JUU YA POINT 3 ZA SIMBA NA KAGERA...WAAMUA HAYA...


Bodi ya Ligi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imewajibu rasmi Simba SC juu ya sakata lao la kupokwa pointi tatu za mezani walizopewa baada ya rufaa yao dhidi ya Kagera Sugar wakidai kumcheza mchezaji Mohamed Fakhi akiwa na kadi tatu za njano.

Kwa mujibu wa barua kutoka katika Bodi ya Ligi zimesema kuwa Fakhi hakuwa na kadi tatu za njano wakati akicheza mchezo dhidi ya Simba uliofanyikia uwanja wa Kaitaba, Bukoba Aprili 2 mwaka huu.

"TFF ambayo ndiyo yenye dhamana ya usimamizi wa mpira nchini na ambayo ndiyo iliyokaimu madaraka kwa TPLB kuendesha ligi kuu iliitisha kikao cha Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ambayo ilichunguza kwa undani sakata hili na baada ya uchunguzi wao ambao walihoji watu mbalimbali, walituandikia kutujulisha kuwa wamebaini mchezaji Mohamed Fakhi anayelalamikiwa na Simba hakuwa na kadi 3 siku ya mchezo wa Kagera Sugara dhidi ya Simba hivyo alikuwa halali kucheza mchezo huo". Ilisema barua hiyo


No comments:

Post a Comment

MAKTABA YA MAGAZETI / NEWSPAPER LIBRARY....... SOMA HAPA MAGAZETI YA SASA NA YALIYOPITA

  • MAGAZETI.
  • Tree in field with blue sky.
  • MAGAZETIt