asali

mbogo

sawe tv

advertise

SLIDE MANENO


Usipitwe na chochote, tupo ili kukuhabarisha tembelea blog hii kila siku, pia usisahau ku subscribe youtube channel yetu ya sawe tv

Thursday, May 11, 2017

HATIMAYE ASKOFU GWAJIMA NA WASAIDIZI WAKE KUHUKUMIWA KWA MAKOSA HAYA

Image result for funga pingu
ASKOFU wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima na wasaidizi wake watatu wanaotuhumiwa kushindwa kuhifadhi silaha na risasi wanatarajiwa kuhukumiwa Julai 31, mwaka huu.

Hukumu hiyo inatarajiwa kutolewa na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha, baada ya jana wakili wa utetezi, Peter Kibatala kueleza kuwa wamefunga ushahidi wao wa mashahidi sita.

Baada ya kueleza hayo, Hakimu Mkeha alisema  anaahirisha kesi hiyo hadi Julai 31, mwaka huu kwa ajili ya kusoma hukumu.

Katika kesi hiyo, upande wa mashtaka uliwakilishwa na Mawakili wa Serikali, Shedrack Kimaro na Joseph Maugo.


No comments:

Post a Comment

MAKTABA YA MAGAZETI / NEWSPAPER LIBRARY....... SOMA HAPA MAGAZETI YA SASA NA YALIYOPITA

  • MAGAZETI.
  • Tree in field with blue sky.
  • MAGAZETIt