asali

mbogo

sawe tv

advertise

SLIDE MANENO


Usipitwe na chochote, tupo ili kukuhabarisha tembelea blog hii kila siku, pia usisahau ku subscribe youtube channel yetu ya sawe tv

Thursday, June 29, 2017

BAADA YA MFUNGO, TRUMP AWAKALIA KOONI TENA WAISLAM, AJA NA KUWAFANYIA JAMBO HILI TATA,,,,TAZAMA HAPA ILIVOKUWA

Rais wa Marekani, Donald Trump ameweka masharti mapya ya maombi ya hati za kusafiria kwa mataifa sita ya Kiislamu na wakimbizi duniani.

Moja ya masharti hayo ni kuwa anayeomba visa lazima awe na uhusiano na mtu mwenye ushirikiano wa kibiashara na Marekani.

Nchi zinazoguswa na masharti hayo ni pamoja na Iran, Libya, Somalia, Sudan Syria na Yemen.

Ujumbe kuhusu masharti hayo umetumwa katika balozi zote za nchi hizo.

Masharti hayo mapya yameanza kutekelezwa jana na yanagusa pia mahusiano ya kifamilia kama mzazi, mkeo ama mumeo, mtoto wa kiume ama wa kike aliye Marekani.

Masharti hayo yanatolewa baada ya Mahakama Kuu nchini Marekani kusitisha  kwa muda agizo la Rais Trump  la kuzuia nchi za Kiislamu kuingia Marekani, zuio ambalo lilikosolewa.


No comments:

Post a Comment

MAKTABA YA MAGAZETI / NEWSPAPER LIBRARY....... SOMA HAPA MAGAZETI YA SASA NA YALIYOPITA

  • MAGAZETI.
  • Tree in field with blue sky.
  • MAGAZETIt