asali

mbogo

sawe tv

advertise

SLIDE MANENO


Usipitwe na chochote, tupo ili kukuhabarisha tembelea blog hii kila siku, pia usisahau ku subscribe youtube channel yetu ya sawe tv

Tuesday, June 27, 2017

SIMBA WAWEKA MEZANI MKATABA WA NGOMA, TAARIFA RASMI HII HAPA

Image result for donald ndombo ngoma
WAKATI kesho Jumatano straika, Donald Ngoma akisubiriwa kutua nchini akitokea kwao Zimbabwe, tayari uongozi wa Simba umeshamuwekea mezani mkataba wa miaka miwili.

Ngoma ambaye msimu uliopita alikuwa akiitumikia Yanga ambayo tayari amemaliza mkataba, msimu ujao anaweza kuvaa jezi za Simba kutokana na timu hiyo kuonesha nia ya dhati ya kuihitaji saini yake.

Mzimbabwe huyo aliyejiunga na Yanga misimu miwili iliyopita, tayari ameshafanya mazungumzo ya awali na Simba huku ikitaarifiwa kwamba yamekwenda vizuri.

Chanzo cha ndani ya Simba, kimesema kuwa baada ya kuwa na asilimia kubwa ya kumnasa Ngoma, tayari wameshaandaa mkataba ili akitua tu asaini.

“Ni kweli Ngoma tunamuhitaji na tayari tumeshaongea nae kila kitu kimekwenda sawa, alisema atawasili baada ya kumalizika kwa Sikukuu ya Idd,” kilisema chanzo hicho.


1 comment:

  1. Kipi ni cha kweli? anakuja Simba au anaenda Polokwane ya South Africa?

    ReplyDelete

MAKTABA YA MAGAZETI / NEWSPAPER LIBRARY....... SOMA HAPA MAGAZETI YA SASA NA YALIYOPITA

  • MAGAZETI.
  • Tree in field with blue sky.
  • MAGAZETIt