asali

mbogo

sawe tv

advertise

SLIDE MANENO


Usipitwe na chochote, tupo ili kukuhabarisha tembelea blog hii kila siku, pia usisahau ku subscribe youtube channel yetu ya sawe tv

Saturday, July 15, 2017

MSIMBAZI SASA KUMEKUCHAA..!!! HATIMAYE UKATILI WA SIMBA WAMWAGWA HADHARANI., TAZAMA UJIONEE MWENYEWE HAPA

Kocha wa Gor Mahia FC, Dylan Kerr, ameelezea masikitiko yake namna alivyofukuzwa kazi na Uongozi wa Simba, baada ya kushindwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Mapinduzi, wakati akiifundisha timu hiyo, miezi 16 iliyopita, huko Zanzibar.

Kerr amesema mipango yake ilikuwa ni kuhakikisha Simba inatwaa ubingwa Ligi Kuu Bara na kama ikishindikana basi amalize akiwa nafasi ya pili.

Kocha huyo amesema kamwe hatawasahau mashabiki na wachezaji wake kwa ukarimu waliomuoneshea wakati akiinoa klabu hiyo, pamoja na kuiamini kazi yake huku akisema atazidi kuwakumbuka.

Kerr amewataja wachezaji baadhi kama Jonas Mkude, Vincent Angban, Peter Manyika, Justice Majabvi, Mohammed Zimbwe au Tshabalala, Mwinyi Kazimoto, kuwa ni mara nyingi amekuwa akiwasiliana nao toka aondoke Simba.


Mwisho kabisa Kerr amewataka wanasimba wote kuendelea kuonyesha umoja ndani ya timu yao, kama kauli mbiu ya Nguvu Moja, namna inavyosema.

Kocha huyo alionekana kuwa kipenzi cha wachezaji wakati akiinoa Simba lakini viongozi hawakufurahishwa naye na walisema hakukuwa na nidhamu ndani ya kikosi chake.

USIKOSE KUTAZAMA VIDEO HII HAPA CHINI



No comments:

Post a Comment

MAKTABA YA MAGAZETI / NEWSPAPER LIBRARY....... SOMA HAPA MAGAZETI YA SASA NA YALIYOPITA

  • MAGAZETI.
  • Tree in field with blue sky.
  • MAGAZETIt