asali

mbogo

sawe tv

advertise

SLIDE MANENO


Usipitwe na chochote, tupo ili kukuhabarisha tembelea blog hii kila siku, pia usisahau ku subscribe youtube channel yetu ya sawe tv

Friday, December 23, 2016

TRUMP ATOA YA MOYONI KUHUSU MAREKANI NA NUCLEAR

 Trump aitaka Marekani kuboresha silaha za nuklia

Donald Trump ameitaka Marekani kuboresha zaidi uwezo wake wa zana za nuklia.

Rais huyo mteule ambaye ataingia ofisini mwezi ujao amesema kuwa Marakani ni lazima ichukue hatua kama hizo, hadi wakati ulimwengu utatathmini suala la nuklia.

Trump aliyazungumza hayo saa kaadha baada ya rais wa Urusi Vladimir Putin kusema kuwa Urusi inahitaji kuboresha uwezo wake silaha za nuklia

Marekania ina silaha 7,100 za nuklia huku Urusi ikiwa inamiliki silaha 7,300 kulingana na shirika la kudhibithi silaha la marekani.

Trump aliyaandika hayo kwenye akaunti yake ya mtando wa twitter

Wakati wa kampeni, Trump alisema kuwa silaha la nuklia ndilo tatizo kubwa zaidi linaloikumba dunia.

Mgombea wa chama cha Democratic Hillary Clinton mara kwa mara alimtaja Trump kuwa mtu asiye na uvumilivu wa kuweza kuzuia vita vya kinuklia.
Putin anasema Urusi ni imara kuliko hasimu wake yeyote


No comments:

Post a Comment

MAKTABA YA MAGAZETI / NEWSPAPER LIBRARY....... SOMA HAPA MAGAZETI YA SASA NA YALIYOPITA

  • MAGAZETI.
  • Tree in field with blue sky.
  • MAGAZETIt