Zari The Bosslady amedai kuwa anataka harusi yake na Diamond Platnumz
iwe kubwa na yenye gharama kuwahi kufanyika Afrika Mashariki.
Hata hivyo, itafanyika baada ya kuwa wamefanya mambo ya muhimu zaidi
ikiwemo kujijenga zaidi walivyo sasa. Akizungumza kwenye kipindi cha Leo
Tena cha Clouds FM Alhamis hii, Zari amedai kuwa suala la kufunga ndoa
sio kitu kinachowapa pressure.
Amedai kuwa hawajawahi kukaa chini na kuwa na majadiliano ya kina
kuhusu ndoa, licha ya hadi sasa kuwa na watoto wawili, Tiffah na Nillan.
Staa huyo wa Uganda amedai kuwa moja ya mambo ambayo wanataka kufanya
ni kuhakikisha kwanza wanawajengea watoto wao apartments zao
zitakazowasaidia katika maisha yao hata kama wazazi wao wasipokuwepo.
Hata hivyo Zari amedai kuwa mwezi March mwaka huu Diamond ataenda
rasmi kujitambulisha kwa baba yake na kuhalalisha uhusiano wao pamoja na
kuomba mkono wa ndoa.
SLIDE MANENO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment