asali

mbogo

sawe tv

advertise

SLIDE MANENO


Usipitwe na chochote, tupo ili kukuhabarisha tembelea blog hii kila siku, pia usisahau ku subscribe youtube channel yetu ya sawe tv

Sunday, February 12, 2017

PICHA: MANJI HOI MAHABUSU ACHUKULIWA NA GARI LA KUBEBA WAGONJWA

Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji amekimbizwa hospitali baada ya kuugua akiwa mahabusu.

Taarifa zinaeleza, Manji ambaye alikuwa mahabusu katika kituo Kikuu cha Polisi cha Dar es Salaam, alianza kuumwa tokea jana.

“Kweli amekimbizwa hospitali na sasa anapatiwa matibabu,” alisema mmoja wa watu wake wa karibu.

Manji alikuwa mahabusu ambako amewekwa tokea Alhamisi iliyopita baada ya kuitwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, akitajwa katika listi ya watu 65 wanaotuhumiwa katika suala la madawa ya kulevya.

Lakini leo ameugua ghafla baada ya kuendelea kubaki rumande kwa siku zote licha ya kwamba hajapelekwa mahakamani.

Kumekuwa na taarifa huenda kesho akafikishwa mahakamani, lakini bado maofisa wa Jeshi la Polisi wamekuwa hawataki kulizungumzia suala hilo.
Kwenye msafara huo ulioondoka gari lake aina ya Range Rover lilikuwepo pia lakini yeye alichukuliwa na gari la Wagonjwa lenye namba za usajili za DFP, muda mfupi ujao nitakuletea video fupi ikionyesha mazingira ya ilivyokua.



No comments:

Post a Comment

MAKTABA YA MAGAZETI / NEWSPAPER LIBRARY....... SOMA HAPA MAGAZETI YA SASA NA YALIYOPITA

  • MAGAZETI.
  • Tree in field with blue sky.
  • MAGAZETIt