asali

mbogo

sawe tv

advertise

SLIDE MANENO


Usipitwe na chochote, tupo ili kukuhabarisha tembelea blog hii kila siku, pia usisahau ku subscribe youtube channel yetu ya sawe tv

Thursday, April 27, 2017

HATIMAYE KAMBA YALEGEZWA KWA KESI YA WANAFUNZI KUTIWA MIMBA..HAYA NDIYO MAPYA YALIYOAMULIWA....

Image result for mwanafunzi mimba
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia ,Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu amesisitiza kuwa wanafunzi wa kike wanaopata mimba wakiwa mashuleni waendelee na masomo yao, ili kufikia malengo walioyanayo nchini.
Waziri Ummy ameyasema hayo leo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kwanza wa masuala ya kijinsia ulioandiliwa na Chuo Cha Ualimu (DUCE) alipomuwakilisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano waa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.
“Tunapokataza watoto wa kike wasiendelee na masomo pindi wanapopata ujauzito wakiwa mashuleni, tunawaadhibu watoto wa masikini washindwe kutimiza malengo yao kwa wakati waliotarajia,”alisema Waziri Ummy.
Kwa upande wa Mkuu wa Chuo cha DUCE, Profesa William Anangisye amesema lengo la mkutano huo ni kuleta chachu ya kuwatia moyo wanafunzi wa kike kupenda masomo ya sayansi ili kupata wanasayansi wanawake nchini.


No comments:

Post a Comment

MAKTABA YA MAGAZETI / NEWSPAPER LIBRARY....... SOMA HAPA MAGAZETI YA SASA NA YALIYOPITA

  • MAGAZETI.
  • Tree in field with blue sky.
  • MAGAZETIt