asali

mbogo

sawe tv

advertise

SLIDE MANENO


Usipitwe na chochote, tupo ili kukuhabarisha tembelea blog hii kila siku, pia usisahau ku subscribe youtube channel yetu ya sawe tv

Monday, January 9, 2017

TAZAMA NDEGE MPYA YA ARSENAL YA KIFAHARI



Arsenal imetambulisha ndege mpya ambayo itakuwa inaitumia kusafiria kwenda kwenye mechi zake za ugenini za Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Ndege hiyo ni ya kifahari na ina kila kitu kinachohitajika ndani. Klabu hiyo iliionyesha ndege hiyo kwenye Instagram wiki iliyopita, aina ya Emir­ates Airbus A380 nje ikiwa im­epambwa na picha za mastaa watano wa timu hiyo; Hector Bellerin, Olivier Giroud, Santi Cazorla, Alexis Sanchez na Mesut Ozil.

Ndani ya ndege hiyo, kila mchezaji ana kitanda chake huku wakiwa wamewekewa anasa kibao, zikiwemo chaneli za televisheni 2,500 na kila mchezaji ana TV yake.
Ndani kuna baa ya kisasa yenye vinywaji vya kila aina, vyoo na mabafu lakini pia maz­ingira mazuri ya kukaa.
The Gunners wataipanda ndege hiyo kwa mara ya kwan­za watakaposafiri kuifuata Bayern Munich mwezi ujao. Angalia picha.







No comments:

Post a Comment

MAKTABA YA MAGAZETI / NEWSPAPER LIBRARY....... SOMA HAPA MAGAZETI YA SASA NA YALIYOPITA

  • MAGAZETI.
  • Tree in field with blue sky.
  • MAGAZETIt